Category: Neno la siku

IBADA YA JUMAPILI – 29.06.2025

MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA 1. Nguvu ya Msalaba 1 Wakorintho 1:18“Kwa maana neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.” Kwa wale wanaopotea, ujumbe wa msalaba ni upuzi, lakini kwa wale wanaookolewa ni nguvu ya Mungu. Lazima uelewe ni nani anayetafakari kuhusu wokovu mara kwa mara wale wanaotafakari kuhusu wokovu mara zote wanakua kiroho, kiakili, na hata kiuchumi. Lakini wale wanaopuuzia wokovu, hata kama wanadai wameokoka, maisha yao yanazidi kudidimia siku baada ya siku, na wanakumbwa na matatizo kwa sababu hawatafakari kuhusu wokovu. Nguvu ya msalaba inakukumbusha jinsi ya kuishi. Lakini

Read More

KUPOKEA ROHO MTAKATIFU

Na, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira- Kanisa la Efatha Matendo ya Mitume 2:38 “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.” Kipawa hutafsiriwa kama kitu kinachotolewa na kukubaliwa bila sharti ikimaanisha tendo la kupokea. Kipawa hakijakamilika mpaka pale mtu apokee kile kilichotolewa bure kwake. Swala la kipawa ni ile hali yako ya kupokea. Tutajua umepokea kipawa kwa kuona udhihirisho; kuna hali fulani, tabia na jambo litachipuka ndani yako. Watu wataanza kuona unapenda kuomba, kusoma Biblia, kwenda Kanisani na kwa njia hiyo unaruhusu Roho Mtakatifu azidi

Read More

Linda sana moyo wako

NENO LA SIKU. Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha. Mithali 4:23 “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.” Mafanikio hayatokani na fedha unazozalisha, wala vitu ulivyonavyo bali yanatokana na wewe ulivyo ndani yako, kama wewe ni mtu wa kushindwa ndani basi utashindwa na nje, lakini kama wewe ni mshindi ndani basi utashinda na nje. Mara zote ibilisi anapenda kukudhoofisha ndani ili uwe mpotezaji nje. Kama kuna kitu unapaswa kukilinda sana ni moyo wako, linda moyo wako maana humo ndimo zilipo Nguvu za mafanikio, Nguvu za ushindi wako zipo hapo. Ndani ya

Read More

Ni wakati wako wa kumiliki

NENO LA SIKU. Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha. Yohana 15:5 “ Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.” Ukikaa katika mzabibu mwema ambaye ni Baba wa mbinguni Yeye atakupa kumiliki lakini ukikaa nje yake yaani katika mzabibu mwitu utazaa matunda ya dunia hii ambayo ni ya uharibibifu na kamwe hautaweza kumiliki milki zako alizokukusudia Baba yako wa Mbinguni. Biblia inasema “maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote”, ukiona kuwa hauwezi kufanya chochote jua kuwa huenda umeokoka

Read More

Tenda kwa ushujaa na uhodari ili upate kumiliki

NENO LA SIKU Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha Tarehe 17/10/2024 Yoshua 1:7 “Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda sawasawa na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu; usiiache, kwenda mkono wa kuume, au wa kushoto, upate kufanikiwa sana kila uendako.” Mafanikio hutokana na Juhudi katika Kazi. Mtu anapofuata maelekezo ya kufanya mambo ili yapate kutokea huingia katika hatua ya Ustawi, asipotenda kwa Ushujaa na Uhodari hawezi kustawi. Mungu alimwagiza Yoshua awe Hodari na Moyo wa Ushujaa ndipo ataweza kuwarithisha Wana wa Israeli Nchi yao ya Ahadi, hii inamaana kuwa kama asingekuwa hodari na mwenye

Read More

Ili ufikie ndoto yako kuna gharama unapaswa kulipa

NENO LA SIKU. Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha. Tarehe 16/10/2024. Mathayo 24:13 “Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.” Wabeba ndoto wana vizuizi vingi sana kutoka kwa wapinzani wao. Kabla ya kuona ndoto yako ikitimia kuna maumivu mengi utapitia ili hiyo ndoto ipate kutimia, kwa sababu NDOTO ni kama mtoto akitoka katika tumbo la mama yake. Usiwe na mashaka unapopitia maumivu ili kuifikia ndoto yako kwa sababu upo katika Njia sahihi. Kabla ya Yusufu kuifikia ndoto yake, alipita kunako maumivu mengi; alitaka kuuawa na ndugu zake, aliuzwa utumwani, alifungwa gerezani lakini aliishia kuwa mtu mkuu

Read More

Haki ya Mungu kwako

NENO LA SIKU. Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha. Tarehe 15/10/2024. Kila mtu huku duniani ana ratiba yake ambayo Mungu amempangia na ili uweze kuvipata vile Mungu alivyokuandalia ni lazima utembee katika kweli ya Mungu ili uweze kuipata haki yako. Mara zote usipende kumuomba Mungu akupe kufanana na mtu fulani? La, kwa sababu unapoomba Mungu akupe kuwa kama mtu fulani ina maana kuwa utapata ambacho sio chako. Mfano; haki ya Daudi ilikuwa afikie kuwa mfalme katika njia aliyopitia yeye; lakini haki ya Yusufu ilikuwa lazima akawe mtumwa katika nyumba ya Potifa, aende jela ndipo akawe mkuu

Read More

Urithi wako umeandaliwa mbele ya adui zako

NENO LA SIKU. Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha. Tarehe 14/10/2024. Zaburi 23:5 “Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, na kikombe changu kinafurika.” Mungu amekukusudia kumiliki ndani ya Mwaka huu wa Kumiliki, lakini meza yako imeandaliwa mbele ya adui zako, pale ambapo watesi wako wapo, sasa usipowashughulikia hao adui zako kamwe hautaweza kumiliki yale yaliyo ya kwako. Mungu akawaambia wana wa Israel amewapa nchi ya maziwa na asali, wapi? Hapo ambapo kuna majitu, walipofika mahali wakakata tamaa na kujiona wao ni kama panzi mbele ya hayo majitu hawakuweza kuirithi ile

Read More

Use well the opportunity of life given to you

DAILY DEVOTION With, Apostle and Prophet Josephat Elias Mwingira- Efatha Church Ecclesiastes 12:1 “Remember now your Creator in the days of your youth, Before the [aldifficult days come, And the years draw near when you say, “I have no pleasure in them.” Don’t wait for someone to encourage you to worship your God, because if you play with the opportunity that God has given you today to worship Him, there will be a day when you will regret it. God doesn’t hear the prayers of the dead but He hears the prayers of the living, if you did not get

Read More

If the foundations are destroyed, what do you do?

DAILY DEVOTION. With, Apostle and Prophet Josephat Elias Mwingira- Efatha Church. Psalms 11:3 “If the foundations be destroyed, what can the righteous do?” You may be wondering why God stands apart from you when you are tempted? It is because your foundations are destroyed. There are people who are very faithful to God, they love God, they serve God but their lives are still a struggle, some are struggling to get school fees for their children, others to find food, etc. If the source of your inheritance is destroyed and the right of possession is destroyed, what do you do?

Read More