Muhtasari Mahubiri Siku ya Pili

MUHTASARI WA SIKU YA 2

Mada: Kusimama katika Nafasi ya Mungu na Kutembea katika Baraka za Kimungu

Siku ya 2 ilijumuisha mafundisho yenye nguvu kutoka kwa Mchungaji James Commey na Mchungaji Jens Garnfeldt kutoka Denmark, ikisisitiza nafasi yetu ya kiroho, mamlaka, na baraka tunazopokea katika Kristo. Lengo kuu lilikuwa kuelewa ni nani sisi katika Mungu, kutembea katika kusudi lake, na kusimama imara katika nafasi ya kiroho aliyotupa.

1. MUNGU ANA NAFASI NA KUSUDI KWAKO (Mchungaji James Commey)

Akirejelea Waefeso 2:6-7, Joshua 1:6, na Esta 4:14, Mchungaji Commey aliwafundisha waumini kuwa Mungu amepanga nafasi ya kipekee kwa kila mtu katika maisha binafsi, huduma, familia, na hatima. Hali mbaya zaidi si kupoteza mali au fursa, bali kupoteza nafasi aliyokupa Mungu.

Aliwahimiza waumini kutembea na Mungu katika mambo mapya yatakayofanya, kuwa hodari na jasiri kama Joshua, na kusimama imara katika wito wao licha ya changamoto. Kwa mfano wa Yusufu, aliwafundisha kuwa magumu mara nyingi hupelekea kukuwa na kutimizwa kwa kusudi la Mungu. Kama Esta, waumini lazima watambue kuwa wako katika nafasi yao “kwa wakati huu maalumu.” Mafundisho yalimalizika kwa wito wa kusimama imara kwa imani, kutoachana nafasi ya kiroho, na kuamini mpango wa Mungu hata katika majaribu.

2. MAMLAKA YA KIUNGU NDANI YA MTU (Mchungaji Jens Garnfeldt)

Akirejea Mwanzo 1:26, Zaburi 8:4-6, na Zaburi 115:16, Mchungaji Garnfeldt alisisitiza kuwa Mungu aliumba binadamu kwa sura yake ili kutawala, kumiliki dunia. Binadamu alipewa heshima na utukufu, na kuwa mwakilishi wa mamlaka ya Mungu. Hata hivyo, kupitia dhambi, Adamu alipoteza mamlaka hiyo, ambayo Shetani aliyapata kwa muda. Yesu Kristo alikuja kwa umbo la mwanadamu kurejesha mamlaka hiyo kisheria.

Kupitia kifo chake na ufufuo, Kristo alikomboa binadamu na kurejesha mamlaka yetu duniani. Waumini sasa ni watawala tena waliyopewa utukufu na heshima. Mchungaji Garnfeldt alisisitiza kuwa Mungu daima hufanya kazi kupitia watu; kila harakati ya kiungu duniani inahitaji chombo ambacho ni binadamu. Alitabiri kuibuka kwa msukumo wa kitaifa nchini Tanzania, akitangaza kuwa Mungu anainua watu watakaobeba utukufu wake kote Afrika.

3. BARAKA ZA MUNGU KATIKA KRISTO YESU (Mchungaji Jens Garnfeldt)

Akihubiri kutoka Waefeso 1:3, Mchungaji Garnfeldt aliwafundisha waumini kuwa Mungu amewabariki kwa baraka zote za kiroho katika mbingu. Baraka ya kweli haipimwi kwa mali bali kwa uwepo na maisha ya Mungu ndani yetu. Baraka hii hutoa nguvu ya kufanikisha, mabadiliko, na matunda ya kiroho.

Alikumbusha kuwa Yesu alichukua laana ili binadamu aweze kuishi katika baraka za Abrahamu. Baraka hii inaleta ongezeko, katika fedha na dhahabu, wanyama, watu, mashamba na mengine kamahayo.

4. UREJESHAJI WA UTAMBULISHO NA HATIMA (Mchungaji James Commey)

Akirejea 2 Timotheo 3:16, Mwanzo 1:26, na 1 Mambo ya Nyakati 4:9, Mchungaji Commey alihitimisha na ujumbe wa kurejesha utambulisho. Neno la Mungu, alisema, ni mwongozo wa kiungu unaounda mtazamo wetu na kurejesha nafasi yetu katika Kristo. Kila mwamini ameumbwa kwa sura ya Mungu si kwa bahati, bali kwa kusudi.

Alitumia hadithi ya Yabes, ambaye alikataa kuishi chini ya maumivu na vizuizi vya jina lake. Vilevile, waumini lazima wakatae utambulisho wa uwongo unaowekwa na hali mazingira au watu. Mungu hubadilisha mtazamo wetu, kama alivyofanya kwa Gideoni na Daudi, na kila neno hasi au laana lililosemwa dhidi yetu linaangamizwa kwa jina la Yesu. Mchungaji Commey aliwahimiza waumini kuinuka, kudai hatima yao ya kiungu, na kutembea katika utukufu wa Mungu.

HITIMISHO

Siku ya 2 ilikumbusha kwa nguvu kuwa:

  • Mungu ana nafasi na kusudi la kipekee kwa kila mtu.
  • Tumeumbwa kwa sura yake ili kutawala na kuonesha utukufu wake.
  • Yesu alirejesha mamlaka yetu na kutuweka katika baraka za Abrahamu.
  • Utambulisho na hatima yetu ya kweli vinaamuliwa na Mungu, si maneno au hali za binadamu.

Waumini walihimizwa kusimama imara, kutembea kwa ujasiri katika wito wao, na kubeba msukumo ambao Mungu anaushikilia katika mataifa.