Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira akiwekwa wakfu na Mtumishi wa Mungu Dr. Morris Cerrulo
KUHUSU KANISA LA EFATHA
Efatha maana yake funguka Marko 7:34
Kanisa la Efatha, zamani (Huduma ya Efatha) lenye msingi wa kitume na kinabii, lilianzishwa mwaka 1996 na kuandikishwa kisheria kama huduma hapa Tanzania mwaka 1997. Mwaka 2021 likapata usajili wa kanisa. Kanisa limeasisiwa na Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, ambaye ndiye Mtume mkuu wa kanisa hili, ambalo linakua kwa kasi hapa Tanzania na nje ya Tanzania.
Kanisa la Efatha ni maono aliyopewa mtumishi wa Mungu, Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, ambaye ndani yake kuna kusudi la Kiungu. Baadhi ya majukumu ya kanisa ni;
- Moja Kuponya watu kutokana na mateso ya magonjwa na madhaifu mbalimbali.
- Pili Kuwafungua watu kutoka kwenye vifungo mbalimbali vya mwili, nafsi na roho.
- Tatu Kuliandaa kanisa la mwisho tayari kwa ajili ya unyakuo.