Naitwa Monica Ambros, nilipata tatizo la kutokwa na damu mfululizo baada ya kujifungua kwa operation, damu ilikuwa nyingi kiasi ambacho ilinilazimu kukalia ndoo ili damu inayotoka iende kwenye ndoo maana ilikuwa nyingi sana. Nilitibiwa hospitali nyingi na kwa waganga wengi wa kienyeji lakini sikupona. Hali hii iliathiri uchumi wetu na mume wangu kwa kiasi kikubwa na ilipofika mwaka jana ndipo nilipoamua kutafuta msaada kwa Mungu.
Namshukuru Mungu nilipata neema nikaletwa katika kanisa la Efatha na nikapokelewa vizuri, nikaambiwa niokoke na baada ya kuokoa ndipo nilipofunguliwa vifungo vyangu na damu ikaacha kutoka. Namshukuru Mungu baada ya kupokea uponyaji hivi sasa uchumi wetu umerejeshwa na ndoa yangu imekuwa na amani na furaha, hakika Mungu anapatikana Efatha.