Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira
Kutafuta Ufalme wa Mungu:
Mathayo 6:33 “Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.”
Watu wa Mungu wana tabia ya kumtafuta Mungu kila wakati. Yesu alituonyesha katika sala ya “Baba Yetu” kwamba tunapaswa kutamani Ufalme wake uje na mapenzi yake yatimizwe hapa duniani.
Waefeso 2:19 “Basi tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu, watu wa nyumbani mwake Mungu.” Tunapomwabudu Mungu na kuishi kwa kuzingatia mambo ya Ufalme wake, tunakuwa sehemu ya familia ya Mungu hata tukiwa hapa duniani.
Kutafuta Ufalme wa Mungu maana yake ni kutafuta kuwa na tabia ya kiungu — tabia ya mbinguni. Hii hutusaidia kuelewa sauti ya Mungu, mapenzi yake, na namna ya kuishi kwa kumpendeza. Bila hiyo, maisha ni ya kuhangaika tu.
Upendo:
1 Wakorintho 16:4 “Mambo yenu yote na yatendeke katika upendo.”
Unapotenda, hakikisha unatenda kwa upendo — si kwa chuki au kisasi. Mungu ni upendo na kama mwana wa Mungu, lazima uishi kwa upendo. Watu wanapokuona, wanapaswa kuuona upendo wa Mungu ndani yako.
1 Yohana 3:1 “Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye.”
Malaika huangalia ni nani anayeishi kwa upendo na wanamjumlisha katika familia ya Mungu. Ukiwa sehemu ya familia hii, Mungu anakutunza kama mtoto wake wa nyumbani.
Neno lenye upendo lina nguvu, linavutia na linaumba uhai. Neno lisilo na upendo huumiza.
Hata unapotumikia wengine, fanya kwa upendo — ndipo utakuwa msaada wa kweli kwa maelfu.