NENO LA SIKU.
Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha.
Tarehe 21/10/2023.
Isaya 45:11 “BWANA, Mtakatifu wa Israeli, na Muumba wake, asema hivi; Niulize habari za mambo yatakayokuja; mambo ya wana wangu, na habari ya kazi ya mikono yangu; haya! Niagizeni.”
Muulize Yeye kwa habari ya mambo yako sio mambo ya shangazi yako na binamu yako, muulize yale aliyoyaandaa kwa ajili yako maana Yeye amesema tumuulize. Mungu ana kila kitu unachokihitaji, huhitaji kwenda Ujerumani ili uwe tajiri bali unahitaji Nguvu za Mungu.
Nguvu ya Mungu ndiyo itakayokusaidia wewe kushinda changamoto unayopitia. Jifunze namna ya kumuuliza Mungu kwa habari ya kesho yako Yeye amesema tumuulize. Tafuta Nguvu ya Nuru kwa sababu hiyo itakusaidia wewe kuchanua na mwisho utapata Uzima wa milele, lakini nguvu ya giza itakusaidia wewe kupata hukumu ya milele na Jehenamu.