NENO LA SIKU.
Na Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Kanisa la Efatha.
Tarehe 9/11/2023.
1 Yohana 5:4 “Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu.”
Imani yetu ina Ushindi dhidi ya haya;-
• Ulimwengu na nguvu zake.
• Dhambi na uovu wote.
• Ibilisi na nguvu zake.
Unapataje Ushindi au Nguvu ya kushinda haya? Imeandikwa kwa njia ya Damu ya Yesu Kristo ambayo ilimwagika msalabani. Tunaipata Damu ya Yesu kupitia toba, unapotubu toba ya kweli Damu inakuja kukusafisha.
Tunahitaji kujua Ushindi wetu uko wapi, Ushindi wetu upo katika Imani yetu na kupitia Msalaba. Hii ina maana kuwa unaweza kuushinda ulimwengu kupitia toba yako. Unapotubu unapatanishwa na yule aliyeshinda ulimwengu ambaye ni Yesu Kristo kupitia Imani yetu. Kwa kadri unavyoishi maisha ya toba ndivyo unavyokuwa Mkuu katika ulimwengu wa Roho.