Naitwa Glory namshukuru sana Mungu wa Efatha kwa ajili ya mtoto wangu anaitwa Neema ambaye alikuwa akitumikishwa kwenye ufalme wa giza kama mchawi pasipo mimi kujua, na tabia hii ya uchawi alijifunza mahali alipokuwa anafanya kazi.
Namshukuru sana Mungu katika mkutano wa maachilio Chalinze, mtoto wangu alionekana akafunguliwa kutoka kifungo hicho cha kichawi akaokoka na baada ya hapo kila wakati wachawi walipotokea katika ulimwengu wa Roho baba yangu wa kiroho Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira alitokea nakuwafukuza. Siku moja mchawi mmoja alikuja kujisalimisha akasema hakika Baba yenu Mwingira ni kiboko, tumemwacha mtoto wenu hatutamtumia tena.